Licha ya kuwepo kwa msemo usemao mwanamke akiwezeshwa anaweza, lakini wapo baadhi yao wanaojiwezesha wenyewe na kufikia malengo ya pale walipokusudia.
Dhana ya kumdharau mwanamke na kuona kuwa hana uwezo wa kuwa kiongozi katika ngazi fulani imeanza kufifia baada ya baadhi ya wanawake kushika nafasi hizo na kuziongoza vyema.
Dhana ya kumdharau mwanamke na kuona kuwa hana uwezo wa kuwa kiongozi katika ngazi fulani imeanza kufifia baada ya baadhi ya wanawake kushika nafasi hizo na kuziongoza vyema.
Wafuatao
ni wanawake 10 ambao wamewahi kushika nafasi za uongozi na wengine kuendelea kushika nafasi hizo.
JULIET KARIUKI.
Huyu ni mkurugenzi mtendaji wa kwanza mwanamke katika Kituo cha uwekezaji Tanzania
(TIC) . Uteuzi wake ulifanywa na Rais Jakaya Kikwete Aprili 12 mwaka huu na
akakabidhiwa ofisi siku hiyohiyo.
- Bi. Kariuki ana shahada ya kwanza ya sheria na ya uzamili, kwenye sheria ni mtalamu wa ubia kati ya serikali na watu binafsi (Public Private Partnership). Aliwahi kufanya kazi katika Chama Cha benki ya Afrika Kusini.
- Ametenguliwa rasmi apo jana na rais wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli baada kushukiwa kuwa hajalipwa mshahara wake kwa miaka mitatu .
MIZINGA
MELU.
- Ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC tangu Machi 20 mwaka huu. Alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Lawrance Mafuru.
- Mzaliwa wa Zambia katika Kijiji cha Mazabuka na ana shahada ya juu ya biashara (MBA), Zambia National Commercial Bank na Standard Chartered Bank.
SAUDA
S. RAJABU.
Naye
ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa juu wa Mkurugenzi Mkuu na Mtendaji Mkuu
(CEO) wa Kampuni ya Ndege ya Precision Air hapa nchini.
- Alianza kutumikia nafasi hiyo Machi Mosi, mwaka huu baada ya aliyekuwa akikalia kiti hicho, Alfonce Kioko kumaliza muda wake.
- Ana shahada ya kwanza ya biashara na sasa yupo mbioni ‘kuchimbua’ shahada ya juu ya biashara. Amewahi kufanya kazi katika mashirika mengine ya ndege kama vile Kenya Airways , Rwanda na Burundi.
BALOZI
LIBERATA MULAMULA.
- Ni balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico. Amewahi kuwa balozi wetu nchini Canada kuanzia mwaka 1999 hadi 2002.
- Amewahi kuteuliwa kuwa mmoja wa wasuluhishi wa mgogoro wa Rwanda. Ni msomi mwenye shahada ya kwanza na ya pili ya sanaa,alisomea Chuo Kikuu cha St. John’s, Marekani, 1989.
MCHUNGAJI
G.RWAKATARE.
- Huyu ni Mchungaji na kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God na mwanzilishi wa shule za St. Mary’s International alizozifungua mwaka 1997.
- Mwanamama aliyeazisha kutuo cha Praise Power Radio 99.2 FM inayoelimisha jamii na kutoa burudani za kiroho.
GETRUDE
MONGELLA.
Alikua
mwanamke wa kwanza kuwa Rais wa Bunge la Afrika, amewahi kuwa Balozi wa
Tanzania nchini India 1991 hadi 1992 na akawa Katibu Mkuu katika Mkutano wa
Wanawake Duniani uliofanyika Beijing nchini China
mwaka 1995.
Aliwahi
kuwa mshauri wa Mkurugenzi Mkuu wa Unesco na aliwatumikia wananchi wa Ukerewe
akiwa ni mbunge kuanzia 2000 hadi 2010.
February mwaka 2008 alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya African Press Organization (APO).
February mwaka 2008 alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya African Press Organization (APO).
ASHA
ROSE MIGIRO.
Asha-Rose
Mtengeti Migiro ni mwanasheria na mwanasiasa, licha ya kufundisha sheria Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, mama huyu aliwahi kuwa mwanamke wa kwanza kuwa Waziri wa
Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania.
- Lakini kikubwa zaidi ni pale alipoteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Juni 2012.
- Baada ya kumaliza muda wake Umoja wa Mataifa, Migiro hivi sasa yupo nchini akiongoza kitengo cha Mambo ya Nchi za Nje cha Chama Cha Mapinduzi.
SUSAN
MASHIBE.
Huyu
ni rubani na ni injinia wa ndege, ni mwanamke wa kwanza nchini kuwa na
elimu hizo alizopatia Chuo Kikuu cha Michigan, Marekani.
- Ni Mwanzilishi na kiongozi wa Tanzanite Jet Centre Ltd, kampuni aliyoianzisha mwaka 2003 ambayo sasa inajulikana kama Via Aviation na inajishughulisha na biashara ya mambo ya anga nchini na barani Afrika.
- Alikutana na Rais Barrack Obama alipokuja nchini hivi karibuni.
JOYCE
MHAVILE.
Ni mkurugenzi mtendaji wa ITV na Radio One kuanzia 1994. Amekiongoza kituo hicho
cha runinga hadi kushika nafasi ya kwanza kwa ufanisi mwaka jana.
- Amebobea kwenye taaluma ya uandishi wa habari.
- Ni mmoja wa wanawake katika Bara la Afrika walioongoza chombo cha habari kwa mafanikio na kuwa mfano kwa wasichana wanaochipukia hivi sasa katika nchi yetu.